Home Uncategorized MOLINGA ACHEKELEA MAISHA YA YANGA,,ATAJA KINACHOMFELISHA

MOLINGA ACHEKELEA MAISHA YA YANGA,,ATAJA KINACHOMFELISHA

DAVID Molinga, mshambuliaji namba moja wa Yanga amesema kuwa anayafurahia masiha ndani ya Yanga kutokana na sapoti anayopewa kutoka kwa mashabiki pamoja na viongozi.

Raia huyo wa Congo ametupia mabao nane ndani ya Yanga iliyo chini ya Kocha Mkuu, Luc Eymael raia wa Ubelgiji.

Molinga anaamini kwamba angekuwa anapewa nafasi ya kuanza kikosi cha kwanza angekuwa na mabao zaidi ya hayo.

“Maisha ndani ya Yanga ninayafurahia kwa kuwa ninapata ushirikiano kutoka kwa wachezaji wenzangu pamoja na viongozi hilo lipo wazi.

“Ninashindwa kufunga mabao mengi kwa kuwa ninatumia muda mwingi nikiwa benchi hayo nimaamuzi ya kocha siwezi kuingilia ila nikipata nafasi nitafunga zaidi,” amesema,” amesema.

Yanga ipo nafasi ya tatu kwenye msimamo ikiwa na pointi 51 imetupia jumla ya mabao 31 kwenye ligi baada ya kucheza mechi 27.

SOMA NA HII  JAMES KOTEI ATAJWA KUMALIZANA NA YANGA MIAKA MIWILI