Home Uncategorized SAFARI YA MABADILIKO YANGA YAPAMBA MOTO

SAFARI YA MABADILIKO YANGA YAPAMBA MOTO


UONGOZI wa Yanga umewaomba mashabiki na wapenzi wa klabu hiyo kuungana katika kuitimiza ndoto ya timu hiyo kuelekea kwenye mabadiliko.

Mshindo Msolla, Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga amesema kuwa anaamini katika malengo ambayo ameyaweka yatatimia kwa timu hiyo kuwa katika mfumo wa mabadiliko ya utendaji.

“Ninaamini katika kusimamia yale malengo ambayo nipo nayo hasa katika uongozi na kwa sasa ndoto kubwa ni kuona kwamba klabu inakuwa katika mfumo wa mabadiliko.

“Kwa kushirikiana na wadhamini pamoja na wadau nina amini hili linawezekana hivyo kikubwa ni kushirikiana katika kuelekea kwenye safari ya mabadiliko,” amesema.

SOMA NA HII  KAZE: HAKUNA MCHEZAJI ANAYEWEZA KUCHEZA MECHI NNE