Home Uncategorized SIMBA: HAKUNA UADUI DHIDI YA YANGA

SIMBA: HAKUNA UADUI DHIDI YA YANGA


UONGOZI wa Simba umesema kuwa hakuna uadui kati yao na Yanga bali ni ushindani tu ndani ya uwanja.

Akizungumza na Saleh Jembe, Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara amesema kuwa wengi wanashindwa kuelewa kwa kudhani kuna uadui.

“Wengi wanashindwa kuelewa kwamba hakuna uadui kati yetu na Yanga zaidi ni kwamba ni ushindani ndani ya uwanja hakuna kingine.

“Kwetu sisi Yanga na Simba sio dini ni klabu tu za mpira, nikiwa kizazi cha tatu chenye uhusiano wa moja kwa moja na Simba  na Yanga, muda wote nawashangaa wanaosema Yanga na Simba ni maadui,” amesema.   

SOMA NA HII  MCHEKA NA NYAVU MATATA AJIPELEKA YANGA, ATAMBA KUTATUA TATIZO PALE KATI