Home Uncategorized SIMBA WAANZA KUPIGA MATIZI LEO KUJIWEKA SAWA KWA AJILI YA LIGI NA...

SIMBA WAANZA KUPIGA MATIZI LEO KUJIWEKA SAWA KWA AJILI YA LIGI NA KOMBE LA SHIRIKISHO


SVEN Vandenbroeck, Kocha Mkuu wa Simba leo amekiongoza kikosi chake kuanza mazoezi kwa ajili ya maandalizi ya kuelekea kumaliza mechi 10 zilizobaki za Ligi Kuu Bara pamoja na mechi za Kombe la Shirikisho.

Simba imefanya mazoezi leo katika uwanja wa Mo Simba Arena uliopo maeneo ya Bunju.

Masuala ya michezo yalisimamishwa na Serikali Machi 17 kutokana na janga la Virusi vya Corona kuvurugavuruga mambo.

Serikali imesema kuwa kwa sasa hali ya maambukizi imepungua hivyo shughuli za michezo zinatarajiwa kuanza Juni Mosi.

Kwenye ligi kuu bara Simba ni vinara wakiwa na pointi 71 baada ya kucheza mechi 28 na kwenye Kombe la Shirikisho wapo ndani ya timu nane ambazo zimetinga hatua ya robo fainali.

SOMA NA HII  JOH MAKINI AWAOMBA WATANZANIA KUENDELEA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI YA VIRUSI VYA CORONA