ULIMWENGU Jules, nyota anayekipiga ndani ya Klabu ya Rayon Sports ya Rwanda anatajwa kuingia kwenye rada za Yanga.
Habari zinaeleza kuwa mpango mkubwa wa mabosi hao wa Jangwani ni kusuka kikosi kazi kwa ajli ya msimu ujao ili kufikia malengo yao ya kushiriki mechi za kimataifa.
Ulimwengu ambaye ni mshambuliaji amesema kuwa hana hiyana iwapo utaratibu utafuatwa yeye atacheza ndani ya Yanga.
“Ninaamini katika uwezo wangu sitashindwa kucheza kikosi cha kwanza kwani kipaji kipo ndio maana hata huku nilipo ninacheza, mambo yakiwa sawa nitacheza Yanga,” amesema.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.