INJINIA, Hersi Said, Mkurugenzi wa Uwekezaji GSM, amesema kuwa watatoa mkwanja wa maana kwa wachezaji ili kuwaongezea morali ya kupambana kubeba taji la Kombe la Shirikisho.
Yanga ipo hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho ambapo kati ya Julai 27/28 itamenyana na Kagera Sugar endapo itashinda itakutana na mshindi kati ya Simba ama Azam FC.
Said amesema:-Tutatoa mkwanja mrefu kwa ajili ya kuwapa morali wachezaji ili wapambane kwa ajili ya kuhakikisha tunabeba taji la Kombe la FA.
“Malengo yetu ni kuona kwamba timu inarejea kimataifa na inashiriki Kombe la Shirikisho Afrika hivyo suala la bonasi hilo lipo kwa wachezaji kuhakikisha ushindi unapatikana,” amesema.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.