Home Uncategorized EYMAEL ALIYEKUWA KOCHA MKUU WA YANGA AKUTANA NA RUNGU JINGINE

EYMAEL ALIYEKUWA KOCHA MKUU WA YANGA AKUTANA NA RUNGU JINGINE

SHIRIKISHO la Soka la nchini Afrika Kusini (SAFA) limemfutia jumla vibali vya kazi Luc Eymael aliyekuwa Kocha Mkuu wa Yanga kufanya kazi ndani ya nchi hiyo.

Eymael Julai 26 baada ya mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Lipuli alisambaza taarifa ambazo zilikuwa zinaonyesha ubaguzi wa rangi na kusema watanzania hawajui soka.

Mchezo huo Yanga ilishinda bao 1-0 lililofungwa na David Molinga ambaye amefikisha mabao 11 ndani ya Ligi.

Tayari Yanga imeshamfuta kazi Eymael jumla kutokana na kitendo hicho na kuomba radhi kwa mashabiki, Serikali na Shirikisho la Soka Tanzania, (TFF).

Kocha huyo pia aliomba msamaha kwa kueleza kuwa alifanya hivyo kutokana na hasira alizokuwa nazo kwa kupitia kipindi kigumu ndani ya Yanga.

SOMA NA HII  SIMBA YAPIGWA KIDUDE KIMOJA CHA NYUMBANI, NJE KIMATAIFA KUISHABIKIA YANGA NA AZAM FC