Home Uncategorized MKAZI WA DAR AIBUKA MSHINDI WA SHINDA GARI MPYA KABISA LEO

MKAZI WA DAR AIBUKA MSHINDI WA SHINDA GARI MPYA KABISA LEO

HATIMAYE mkazi wa Dar es Salaam, Didas Marik (42), leo Julai 1, 2020 amefanikiwa kuibuka mshindi wa zawadi kubwa ya gari aina ya Toyota FunCargo katika droo kubwa ya Bahati Nasibu ya Jishindie Gari iliyochezeshwa na Kampuni ya Global Publishers katika Viwanja vya Mabibo Sokoni jijini Dar na kuhudhuriwa na watu mbalimbali akiwemo Mkaguzi wa Bodi ya Michezo ya Bahati Nasibu, Elibariki Sengasenga.



Bahati nasibu hiyo iliyokuwa ikiendeshwa kupitia magazeti namba moja ya michezo Tanzania kutoka Global Publishers, Spoti Xtra na Championi, ilidumu kwa takribani miezi mitatu ambapo ilizinduliwa Februari 27, mwaka huu na kuhitimishwa jana Julai Mosi, 2020. 

SOMA NA HII  Cech arejea Chelsea bila ya ‘Helmet’ yake!