Habari za Yanga
Uncategorized

SARPONG ACHEKELEA KUIBUKIA YANGA, ATOA AHADI HII

admin August 23, 2020 9:47 am


MICHAEL Sarpong mchezaji mpya wa Klabu ya Yanga amesema kuwa anafurahi kujiunga na Yanga na anaamini kwamba atapambana kufikia malengo ya timu hiyo.

Sarpong raia wa Ghana yeye ni mshambuliaji amemalizana na Yanga kwa dili la miaka miwili na anatarajiwa kutambulishwa rasmi Agosti 30 kwenye kilele cha Wiki ya Wananchi Uwanja wa Mkapa.


Anaungana na wachezaji wengine wawili ambao ni Tusila Kisinda na Tunombe Mukoko ambao wanatarajiwa kuanza rasmi mazoezi kesho, kuungana na wachezaji wenzao ambao tayari walishaanza mazoezi tangu Agosti 10.


Nyota huyo amesema:”Ninafurahi kuwa mwanafamilia wa Yanga ninatambua kwamba ni timu kubwa na ina wachezaji wengi wazuri hivyo nitakachofanya ni kutimiza majukumu yangu kwa kushirikiana na wachezaji wenzangu.” 

KOCHA MPYA BARCA AWAFUNGULIA MLANGO SUAREZ, BUSQUETS, JORDI ALBA NAMUNGO WATUMA UJUMBE HUU KWA AZAM FC

Deprecated: File Theme without comments.php is deprecated since version 3.0.0 with no alternative available. Please include a comments.php template in your theme. in /home/sokalabo/public_html/wp-includes/functions.php on line 6170

Leave a Reply