Home Uncategorized ANAANDIKA HAJI MANARA AKIWAOMBA WATANZANIA WAMPE JAPO HESHIMA

ANAANDIKA HAJI MANARA AKIWAOMBA WATANZANIA WAMPE JAPO HESHIMA

 

OFISA Habari wa Simba, Haji Manara amewaomba mashabiki na watanzania wampe heshima kabla hajatangulia mbele za haki kwa kuwa amefanya mengi makubwa kwa sasa katika kuutangaza mpira.


Haji ameandika namna hii:-Watanzania nipeni heshima yangu walau kidogo, ntaumia sana nikifa mkaja kusoma salaam zenu makaburini kunielezea wasifu na sifa zangu,huku mkinipamba kwa tenzi na shairi nzuri nzuri.

“Leo Yanga wametumia washehereshaji watano katika jambo ambalo nalifanya peke yangu always!

“Mimi napenda heshima tu ,,msinisifu ila mtambue nimewachangamshia mpira wenu, waliokuwa baridi nimewafanya walau nao wachangamke,japo bado wanafanya uchale tu mbele ya Simba.

“Wanasimba wenzangu tujishukuru kwa tulipo na wenzetu walipo,,.hawana chembe ya ‘Creativity’,(ubunifu),hawajui hata ‘wat they want'(nini wanataka).

“Hebu nyie na Watanzania wote nipeni japo heshima yangu na management ya Simba pamoja na Bodi ya Klabu chini ya tajiri wa mpira bwana MO kwa haya tuliyoyafanya kwa mpira huu ndani ya nchi hii!

“Leo Afrika nzima inazungumzia Simba Day,labda Kesho itazungumza kuhusu anguko la Commandoo wa kimakonde ‘but behind it’ (nyuma yake) kuna kazi kubwa imefanyika.

“Na hiyo kazi imefanyika kutokea Simbaa.Narudia mimi napenda sifa ila nazitaka sasa, sifa niikiwa kaburini au katika jeneza kwangu ni naniliu tu.

“Akili zangu za usiku nazijua mwenyewe.”

SOMA NA HII  FRED MINZIRO AKUNJA JAMVI NDANI YA SINGIDA UNITED