Home Uncategorized BREAKING:AZAM YAMFANYIA VIPIMO MTUPIAJI WA COASTAL UNION

BREAKING:AZAM YAMFANYIA VIPIMO MTUPIAJI WA COASTAL UNION

.
AYOUB Lyanga,kiungo mshambuliaji leo amefuzu vipimo ndani ya Klabu ya Azam FC inayonolewa na Arstica Cioaba.

Nyota huyo alikuwa chini ya Juma Mgunda ambapo kwa msimu wa 2019/20 akiwa Coastal Union alitupia jumla ya mabao nane.

 Baada ya kufuzu vipimo vya afya leo Agosti 2 yupo tayari kabisa kumaliza taratibu za kujiunga na Azam FC, kuelekea msimu ujao.

Saa chache zijazo anatarajia kusaini rasmi mkataba wa  kuitumikia timu hii yenye maskani yake ndani ya viunga vya Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

SOMA NA HII  MBAYA WA YANGA NA KABWILI SIMBA AENDELEA KUWEKA REKODI