KUTOKA Shirikisho la Soka Tanzania,(TFF) wana familia watatu kwenye michezo watapewa malalamiko yao na wito kwa njia ya maandishi ili kuhuduhuria kikao cha Kamati ya Maadili, wanafamilia hao ni:-Mjumbe wa Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya TFF, Zakaria Hans Poppe, Mkuu wa Idara ya Habari wa Klabu ya Simba, Haji Manara na mchezaji Bernard Morrison.
Pia Sekretarieti ya TFF imempeleka Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Klabu ya Yanga, Hassan Bumbuli katika Kamati ya Maadili kwa kutoa taarifa ya uongo.