Home Uncategorized HIVI NDIVYO SIMBA ILIVYOIPIGA BAO AL AHLY

HIVI NDIVYO SIMBA ILIVYOIPIGA BAO AL AHLY

 


KLABU ya Simba imezifunika timu nyingi Afrika ikiwa ni pamoja na Klabu ya Al Ahly ya Misri kutokana  na kushika namba moja kwenye Mtandao wa Istagram.


Hiyo ni kwa mujibu wa Mtandao wa Deporfinanzas ambao umetoa takwimu za mwezi Agosti na kuiweka Simba namba moja kwa umaarufu kutokana na kutembelewa sana na watu.


Takwimu zinaonyesha kwamba kwa mwezi huo watu milioni 536 waliitembelea akaunti ya Simba huku ile ya Al Ahly ilitembelewa na watu milioni 517 na Raja Casablanca watu milioni 511.


Mtandao huo uliandika hivi:”Simba SC ndiyo Klabu maarufu Afrika ndani ya Istagram kwa mwezi Agosti. 


“Hii ni mara ya Kwanza kwa timu kutoka Tanzania kufanya hivi,”.

SOMA NA HII  JIPATIE NAKALA YAKO YA BETIKA BURE KABISA