Home Uncategorized LIVERPOOL YAMALIZANA NA MKATA UMEME THIAGO, MIAKA MINNE

LIVERPOOL YAMALIZANA NA MKATA UMEME THIAGO, MIAKA MINNE


 KLABU ya Liverpool imethibitisha kuwa imepata saini ya nyota wa Bayern Munich, Thiago Alcantara kwa dili la miaka minne.

Kiungo huyo raia wa Hispania kwa sasa atakuwa ni mali ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu England ambao waliutwaa msimu uliopita baada ya miaka 30 kumeguka.

Thamani ya nyota huyo inatajwa kuwa pauni milioni 25 na Liverpool imefikia makubaliano mazuri na mabingwa hao wa Ujerumani hivyo msimu huu wa 2020/21 atakuwa ndani ya Anfield.

Thiago amesema:”Nadhani ni maajabu kwangu ndizo hisia ambazo ninazo. Nilisubiri kwa muda mrefu hatimaye imeweza kutimia, nina furaha kubwa kuwa hapa.

“Kadri muda unayokwenda unatamani kushinda zaidi na ukishinda unahitaji kushinda tena zaidi. Ninafikiria kwamba klabu ina malengo makubwa nami pia ninahitaji kufikia mafanikio hayo na kushinda mataji zaidi.”

SOMA NA HII  ROBERTINHO AJA NA MKAKATI HUU SIMBA SC