Home Uncategorized SHIBOUB AKUNJA MKWANJA WA MAANA KWA WAARABU

SHIBOUB AKUNJA MKWANJA WA MAANA KWA WAARABU

 

SHARAF Shiboub kiungo wa zamani wa Simba ambaye ametwaa mataji matatu msimu wake wa kwanza wa 2020/21 atakipiga ndani ya Klabu ya CS Costantine ya Algeria.

Nyota huyo raia wa Sudan kwa msimu wa 2019/20 alitwaa taji la Kombe la Shirikisho, Ligi Kuu Bara na Ngao ya Jamii.


Mkataba wake wa mwaka mmoja ndani ya Simba ulikamilika na hakuongezewa dili jingine na mabosi wa  Simba hivyo ameibuka ndani ya timu yake mpya akiwa ni mchezaji huru.


Inaelezwa kuwa dau lake ni milioni 600 za Kibongobongo baada ya waarabu wa Algeria kuweka mkwanja huo ambao ni sawa na dola 300,000.


Akiwa Simba ndani ya Ligi Kuu Bara alifunga mabao mawili sawa na yale ya kwenye Ngao ya Jamii aliyofunga mbele ya Azam FC huku akitoa jumla ya pasi sita za mabao.

SOMA NA HII  BRUNO FERNANDEZ REKODI ZAKE NI BALAA, UTD KUFUZU 16 BORA. BASHIRI MERIDIAN BET