Home Uncategorized TIMU YA MBWANA SAMATTA MZIGONI, VPL, SERIE A RATIBA HII HAPA

TIMU YA MBWANA SAMATTA MZIGONI, VPL, SERIE A RATIBA HII HAPA

 


LEO Septemba 20, Ligi Kuu Tanzania Bara inaendelea ambapo ipo mzunguko wa tatu mechi mbili zitapigwa kwa kila timu kusaka pointi tatu muhimu.


Mwadui FC ambayo imecheza mechi mbili na kuambulia kichapo cha mabao mawili inakutana na KMC ambayo imeshinda mechi zake zote mbili za mwanzo kwa msimu wa 2020/21.


Mchezo huu utapigwa leo Septemba 21, Uwanja wa Mwadui Complex wenyeji wakiwa ni Mwadui.


Ruvu Shooting ikiwa imetoka kupoteza kwa kufungwa bao 1-0 mbele ya Ihefu Uwanja wa Sokoine leo Septemba 21 inamenyana na Gwambina FC ambayo imetoka kulazimisha sare ya bila kufungana na Kagera Sugar, itakuwa ni Uwanja wa Mabatini. 


Premier


Aston Villa ya Mbwana Samatta ambaye haelewi hatma yake leo itamenyana na Sheffield majira ya saa 2:00 usiku.


Wolves wao watamenyana na Manchester City.


Serie A


AC Milan itamenyana na Bologna majira ya saa 3:45 usiku.

SOMA NA HII  MNYARWANDA YANGA ASHUSHWA KWA MILIONI 40,SIMBA YASHTUKA, NDANI YA CHAMPIONI JUMATANO