Home Uncategorized JINA LA KELVIN YONDANI LATAJWA YANGA

JINA LA KELVIN YONDANI LATAJWA YANGA


KOCHA mpya wa Yanga, Mrundi, Cedric Kaze amemtaja aliyekuwa beki wa Yanga, Kelvin Yondani kuwa ni mmoja kati ya wachezaji wenye heshima kubwa kwake na alitamani kufanya naye kazi ndani ya timu hiyo.

 

Kocha huyo aliwasili jana usiku kwa ndege ya Shirika la Ndege la Uholanzi (KLM) akitokea nchini Canada tayari kwa kuanza majukumu mapya ndani ya timu hiyo akichukua nafasi ya Mserbia, Zlatko Krmpotic aliyetimuliwa kutokana na mwenendo mdogo wa timu hiyo licha ya matokeo ya ushindi kwenye mechi zake.


Akizungumza na Championi Ijumaa, Kaze alisema kuwa amewafuatilia wachezaji wote wa timu hiyo huku akimtaja Yondani kama ni mmoja wa mabeki bora na mwenye nidhamu ambaye alitamani kufanya naye kazi.

 

“Nimefuatilia wachezaji Yanga ambao walikuwepo tangu awali hata akina Juma Abdul ambao wameondoka pamoja na nahodha Kelvin Yondani wengine wakiwa akina Deus Kaseke, Juma Mahadhi, Fei toto, Ramadhani Kabwili, akina Metacha Mnata, nimewafuatilia wote wa Yanga wanafika 50.


“Yondani ni mchezaji mzuri ambaye amefanya mambo makubwa ndani ya Yanga.Natumia fursa hii kumshukuru kabisa hata rafiki yake akisikia amwambie mwalimu Kaze, anashukuru mchango wake ndani ya Yanga.


“Najua kila kitu katika maisha huwa na mwanzo na mwisho wake, kitu ambacho anapaswa kutambua ni kwamba yeye ni mchezaji mwenye nidhamu kubwa kwenye timu yetu, nilitamani angekuwepo lakini ndiyo hivyo mambo hayakwenda sawa,” alisema Kaze.

SOMA NA HII  POVU LA MASHABIKI YANGA BAADA YA SIMBA KUTUPWA NJE CAF - VIDEO