Home Uncategorized KUMBE MWINYI ZAHERA ALIIBUKIA KAMBI YA YANGA

KUMBE MWINYI ZAHERA ALIIBUKIA KAMBI YA YANGA


 ALIYEWAHI kuwa Kocha wa Yanga, Mwinyi Zahera,  inaelezwa kuwa alivamia kambi ya timu yake hiyo ya zamani kwa ajili ya kwenda kusalimia wachezaji wa timu hiyo pamoja na kocha Cedric Kaze muda mfupi kabla ya mechi yao.

 

Yanga ikiwa jijini Mwanza iliweka kambi katika Hotel ya Capri Point, kwa ajili ya mechi zake tatu za Kanda ya Ziwa, ambapo  ilimalizia mechi yake kwa kuivaa Gwambina FC ambapo Zahera ni mkurugenzi wa benchi la ufundi la timu hiyo.

 

Zahera aliifundisha Yanga msimu uliopita kabla ya kuondolewa kikosini hapo ambapo alikuwa ni miongoni mwa makocha wenye hamasa kubwa ndani ya kikosi hicho ambacho kilikuwa na ukata wa hali ya juu kulikomsababisha aanzishe mpango wa kutembeza bakuli kwa wadau.


Taarifa zimeeleza kuwa Zahera alifika Capri Point asubuhi ya saa 2:30 ikiwa ni muda mfupi kabla ya kuvaana na Yanga katika Uwanja wa Gwambina.

 

Aidha Zahera alipata fursa ya kusalimiana na viongozi wa benchi la ufundi pamoja na baadhi ya wachezaji ambao aliwaacha kikosini hapo huku akiwa na furaha kubwa kuwaona wenyeji wake hao wa zamani na kupata nafasi ya kuzungumza mambo mawili matatu.


Kwenye mchezo huo uliochezwa Uwanja wa Gwambina, ngoma ilikamilika kwa sare ya bila kufungana.

SOMA NA HII  WIMBO MPYA WA YANGA HUU HAPA - VIDEO