Mabao 9 yamekusanywa leo Desemba 18 Kwenye mechi tatu za mwanzo ndani Ligi Kuu Bara.
Mchezo mmoja umekamilika kwa sare ya kufungana bao 1-1 huku mechi mbili timu mbili zikisepa na pointi tatu na mabao matatu.
Ilikuwa namna hii:-
Mwadui 1-1 Polisi Tanzania, Uwanja wa Mwadui Complex.
Kagera Sugar 3-1 Coastal Union, Uwanja wa Kaitaba.
Biashara United 3-0 Mbeya City, Uwanja wa Karume.
Mchezo unaofuata usiku saa 1:00 ni Azam FC v Ruvu Shooting, Uwanja wa Azam Complex.