Home Azam FC AZAM FC YAINYOOSHA KMC MABAO MATATU AZAM COMPLEX

AZAM FC YAINYOOSHA KMC MABAO MATATU AZAM COMPLEX

 VIVIER Bahati,  kocha msaidizi wa Klabu ya Azam FC amesema kuwa bado vijana wake wanazidi kuimarika jambo ambalo limewafanya waibuke na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya KMC.

Azam FC iliibuka na ushindi huo kwenye mchezo wa kirafiki uliochezwa jana Januari 29, Uwanja wa Azam Complex. 

Mabao ya Azam FC mawili yalifungwa na Prince Dube na moja lilipachikwa na Mudhathir Yahya huku lile la KMC likipachikwa na Lusajo Mwaikenda aliyepachika bao hilo kwa penalti.

Bahati amesema:”Ulikuwa ni mchezo mzuri na kila mchezaji alikuwa kwenye wakati mzuri jambo ambalo limetufanya tuwe katika wakati mzuri kwa ajili ya mechi za Ligi Kuu Bara ambazo zinakuja,”.

SOMA NA HII  AZAM FC YAWAWEKA KANDO WAARABU