Home Ligi Kuu MTIBWA SUGAR AKILI ZOTE NI LIGI KUU BARA

MTIBWA SUGAR AKILI ZOTE NI LIGI KUU BARA


UONGOZI wa Mtibwa Sugar umeweka wazi kwamba utapambana kufanya vizuri ndani ya Ligi Kuu Bara kwenye mzunguko wa pili.

Mtibwa Sugar ipo chini ya Kocha Mkuu, Hitimana Thiery ambaye ameibuka ndani ya kikosi hicho baada ya kupigwa chini na kikosi cha Namungo FC

Ofisa Habari wa Mtibwa Sugar, Thobisa Kifaru amesema kuwa watafanya kazi kwa uzuri ili kupata matokeo mazuri.

“Kwa sasa maumivu ya kupoteza Kombe la Mapinduzi, tumeweka kando kabisa akili yetu sasa ni ndani ya Ligi Kuu Bara.

“Tunajua mzunguko wa pili utakuwa mgumu na kila timu inasaka matokeo hivyo nasi tutapambana kufanya vizuri,” .


SOMA NA HII  SAMATTA:TUTAKUJA KIVINGINE MBELE YA SIMBA