Home Uncategorized SIMBA YATUMA SALAMU KWA MTIBWA SUGAR

SIMBA YATUMA SALAMU KWA MTIBWA SUGAR

 


MIRAJ Athuman, kiungo mshambuliaji wa Klabu ya Simba amesema kuwa anaamini kwamba leo wataibuka na ushindi mbele ya Mtibwa Sugar. 


Simba itakutana na Mtibwa Sugar kwenye mchezo wa Kombe la Mapinduzi unaotarajiwa kuchezwa majira ya saa 8:15, Uwanja wa Amaan.


Msimu wa 2020, Simba ilipoteza kwa kufungwa bao 1-0 dhidi ya Mtibwa Sugar mchezo wa fainali na kuifanya timu hiyo kukosa Kombe la Mapinduzi. 


Sheva amesema:”Tunajua Mtibwa Sugar ni timu nzuri na inafanya vizuri ila tutapambana kupata ushindi,”.

SOMA NA HII  SIMBA YATOA TAMKO SAKATA LA KICHUYA