Waamuzi wanne ambao ni raia wa Afrika Kusini, ndiyo wamepewa dhamana ya kuamua mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika kati ya Simba dhidi ya Al Merrikh.
Mchezo huo wa nne kwa timu hizo zilizo kwenye kundi A la michuano hiyo, utapigwa katika dimba la Mkapa jijini Dar es Salaam Machi 16 yaani Jumanne ijayo.
Waamuzi hao ni;
Refa:Victoria Miguel Gomez
1: Zakhele Thusi Siwele
2: Athenkosi Ndongeni
3: Thando Ndzandzeko
Simba inaongoza msimamo wa kundi hilo, wakiwa tayari wamejikusanyia pointi saba katika michezo yao mitatu ambayo wamecheza mpaka sasa.