Home Taifa Stars WACHEZAJI TAIFA STARS MNA DENI LA KULIPA UWANJANI

WACHEZAJI TAIFA STARS MNA DENI LA KULIPA UWANJANI


WACHEZAJI wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars chini ya Kocha Mkuu, Kim Poulsen wameanza maandalizi kwa ajili ya mechi za kuwania kufuzu AFCON.

Machi 25 wanakibarua cha kusaka ushindi mbele ya Equatorial Guinea kwenye mchezo ambao Stars itakuwa ugenini.

Utakuwa mchezo mgumu kwa kuwa kila timu inapeleka wachezaji uwanjani ikihitaji ushindi hapo hesabu lazima ziwe kubwa kwa Stars.

Furaha ya mashabiki ni kuona timu inapata ushindi na ushindi unapatikana kwa maandalizi mazuri ndani ya uwanja. Kwa wakati ambao upo ni lazima kujipanga na kufanya kazi kwa juhudi ndani ya uwanja.

Ikiwa wachezaji mtashindwa kujituma kwenye kusaka ushindi itakuwa ni rahisi kwenye kukwama kufikia malengo yenu. Na kushindwa kufikia malengo ya kupata ushindi ni pigo kwa taifa.

Mkiwa kwenye jambo la kuwakilisha nchi kwenye mashindano ya kimataifa hapo kazi ni moja kupeperusha bendera ya Tanzania bila kuogopa ndani ya uwanja.

Ukweli upo wazi kwamba kila mchezaji ambaye ameitwa kuitumikia timu ya taifa upo wazi na hali hiyo imepeleka kila mmoja akapata nafasi ya kuitwa kikosini kupambana na timu kwa ajili ya majukumu ya Tanzania.

Jambo la kuzingatia ni nidhamu na kuwa wasikivu kwa kile ambacho mwalimu anawaambia. Ikiwa mtafuata maelekezo ya benchi la ufundi itaongeza nguvu na ari kwa mashabiki kuendelea kuwafuatilia kwenye mechi zenu zote.

Imani yetu ni kwamba mnaweza kufanya makubwa ndani ya uwanja  kwa kuwa uwezo mnao na hilo lipo wazi. Uwezo wenu unapaswa utumike kwa ajili ya kupambania taifa letu ambalo linapenda kufuatilia mpira.

Nguvu kubwa itumike katika kuelewa kile ambacho mnafundishwa na kukifanyia kazi ndani ya uwanja. Muda wa maandalizi ni muda pekee wa kurekebisha makosa ambayo mnayafanya ndani ya uwanja.

Hii itazidi kuwafanya mzidi kuwa sokoni kwa kuwa kadri mnavyofanya vizuri mnazidi kuwa kwenye ramani ya kuwa sokoni hasa kwa wale ambao wanawafuatilia.

Wachezaji pambaneni bila kuchoka ndani ya uwanja ili kuweza kufanya vizuri. Ushindani upo wazi ndani ya uwanja nanyi pia ongezeni juhudi katika kusaka matokeo.

SOMA NA HII  KUELEKEA MECHI DHIDI YA DRC CONGO...STARS WATOA AHADI YA KIBABE...'CANNAVARO' ALIOTA KOMBE LA DUNIA...

Jambo kubwa la kufanya ni kukubali kujifunza na pale ambapo mnakosea ndani ya uwanja mna kazi ya kurkebishana wenyewe kwa wenyewe ili kusaka matokeo kwenye mechi zenu ambazo mtacheza.

Kila mchezaji anapenda kuona timu inapata matokeo mazuri. Ikiwa morali itakuwa kubwa kwa kila mchezaji itaongeza nguvu pia ya kupata matokeo mazuri wakati ujao kwenye mechi za ushindani.

Ikumbukwe kwamba wakati timu ikiwa Kenya mchezo wa kwanza wa kirafiki ilipoteza kwa kufungwa mabao 2-1.

Mchezo wa pili ulifutwa na Shirikisho la Soka Tanzania, (TFF) kwa sababu ya kifo cha Rais wa awamu ya tani, John Magufuli ikiwa ni sehemu ya maombolezo kwa shujaa ambaye alikuwa ni mpenda michezo.

Imani yangu ni kwamba wachezaji mtazidi kupambana kwa ajili ya mechi zote za ushindani kitaifa na kimataifa. Kikubwa ni kuongeza juhudi na kufanya kazi kwa kujituma ndani ya uwanja.

Ligi pia kwa sasa ipo kwenye mzunguko wa presha ambapo kila timu imekuwa ikihaha kufikia malengo yake ndani ya uwanja.

Msimu huu tunaona kwamba umekuwa ni wa tofauti kidogo kwa namna kasi yake inavyokwenda ni muhimu kuweza kujifunza kwa ajili ya yale makosa ambayo yanatokea ndani  ya uwanja.

Kwa kufanya vizuri kwa wachezaji kwenye mechi hizi ni fursa ya kuweza kupata nafasi kwenye timu ya Taifa Stars kwa kuwa mwalimu amekuwa akifuatilia na rekodi kwa timu husika na nyingene amekuwa akipewa.

Makosa ambayo yemekuwa yakiripotiwa ni muhimu kufanyiwa kazi kwa kuwa jambo la msingi ni kuona kwamba timu inapata matokeo chanya bila makelele yoyote ndani ya uwanja.