BAKARI Mwamnyeto, beki chipukizi ndani ya Coastal Union iliyo chini ya Juma Mgunda amesema kuwa siri kubwa ya kiwango chake ni juhudi pamoja na nidhamu ndani na nje ya uwanja.
Mwamnyeto amekuwa bora ndani ya Coastal Union ambapo ikiwa imecheza mechi 28 imeruhusu kufungwa mabao 19.
“Kikubwa ni nidhamu nje ya uwanja na ndani ya uwanja ni mambo ambayo yananifanya ninakuwa katika ubora wangu muda wote kwani hakuna kinachowezekana ikiwa hautaweza kufuata ile miiko iliyowekwa,” amesema.
Beki huyo inaelezwa kuwa anawindwa na Simba pamoja na Yanga ambao wanahitaji saini yake huku dau lake likitwaja kuwa ni milioni 100.
Sign in
Welcome! Log into your account
Forgot your password? Get help
Password recovery
Recover your password
A password will be e-mailed to you.