Home Uncategorized YANGA YAMKUMBUKA GHAFLA MAKAMBO

YANGA YAMKUMBUKA GHAFLA MAKAMBO


JUMA Abdul, nahodha wa Yanga amesema kuwa anakubali uwezo wa Heritier Makambo atafurahi pale atakapojiunga na kikosi hicho msimu ujao.

Makambo alikipiga ndani ya Yanga msimu wa 2018/19 ambapo alikuwa ni namba moja kwa kutupia ndani ya klabu hiyo baada ya kufunga mabao 17.

Kwa sasa yupo zake anakipiga ndani ya Horoya na inaelezwa kuwa Yanga ipo kwenye mpango wa kumrejesha mshambuliaji huyo.

“Miongoni mwa washambuliaji ambao walikuwa wanafanya vizuri ndani ya Yanga ni pamoja na Makambo iwapo atarejea nina imani ataendelea na lile balaa ambalo alianzisha.” amesema.

SOMA NA HII  MASHABIKI WA SIMBA KINDAKINDAKI WAKOMAA NA WACHEZAJI HAWA