Home kimataifa PSG YAIVUA UBINGWA WA UEFA CHAMPIONS LEAGUE BAYERN MUNICH

PSG YAIVUA UBINGWA WA UEFA CHAMPIONS LEAGUE BAYERN MUNICH

 


LICHA ya Mabingwa watetezi wa taji la UEFA Champions League kushinda bao 1-0 mbele ya PSG katika mchezo wa robo fainali ya pili ndoto zao za kutetea taji hilo zimekwama mazima.

Mabingwa hao ambao walitwaa taji mwaka 2020 kwa kushinda dhidi ya PSG, wamevuliwa ubingwa na wapinzani wao waliokutana nao zama wakitwaa ubingwa.

Bao la ushindi la Bayern Munich lilipachikwa na Eric Maxim Choupo-Moting dakika ya 40 na kufanya aggregate kuwa 3-3 kwa sababu mchezo wa robo fainali ya kwanza PSG ilishinda kwa mabao 3-2.

PSG inayonolewa na Kocha Mkuu, Mauricio Pochettino inasonga hatua ya nusu fainali kwa faida ya bao la ugenini. Kwenye mchezo huo uliochezwa Uwanja wa Parc des Princes, Neymer aliibuka kuwa mchezaji bora wa mchezo huo na hakuamini kile alichokiona.

Nusu fainali PSG inaweza kukutana na Manchester City ama Borussia Dortmund.


SOMA NA HII  MFAHAMU STAA MKUBWA WA SOKA DUNIAN ANAYELIPWA BILION 26 LAKINI BADO ANAISHI KWA WAZAZI WAKE...