Home Simba SC BOCCO ASEPA NA TUZO YA MCHEZAJI BORA

BOCCO ASEPA NA TUZO YA MCHEZAJI BORA

NAHODHA wa Klabu ya Simba John Bocco ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa mwezi wa tano (Mei) wa Klabu ya Simba (Emirate Aluminium Simba Fans Player of the Month).

Bocco ameshinda tuzo hiyo baada ya kushinda kwa asilimia 59.3 na kuwashinda Benard Morrison aliyepata asilimia 29.4.

Pia mwingine ni Thadeo Lwanga aliyepata asilimia 11.3. Bocco atakabidhiwa tuzo na fedha taslimu 1,000,000 kutoka Emirate Aluminium kama zawadi za mshindi.

Mchezaji wa kwanza kusepa na tuzo hiyo ni Luis Miquissone ambaye ni kiungo aliyepita alikuwa ni Clatous Chama mwamba wa Lusaka.

SOMA NA HII  MIQUISSONE AIWEKEA NGUMU SIMBA....MSHAHARA ANAOTAKA UNAMLIPA CHAMA MARA NNE...