NAHODHA wa Mwadui FC, Mussa Mbissa amesema kuwa wamejipanga kwa ajili ya mchezo wa kesho dhidi ya Yanga utakaochezwa Uwanja wa Mkapa.
Mbissa ameongeza kuwa kesho wataingia kwenye mchezo huo kama fainali licha ya kuwa kwenye mstari wa kushuka daraja kwa msimu wa 2020/21.
Ameongeza kuwa kosa ambalo alifanya na kufungwa kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya Yanga ameshasahau na ameandaliwa kisaikolojia.