Home Azam FC AZAM FC KAZINI LEO KAGAME CUP, AZAM COMPLEX

AZAM FC KAZINI LEO KAGAME CUP, AZAM COMPLEX


AZAM FC leo itakuwa na kibarua cha kusaka ushindi mbele ya Big Bullets ya Malawi katika mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Kagame.

Ni majira ya saa 1:00 usiku, Uwanja wa Azam Complex mchezo huo unatarajiwa kuchezwa kwa timu zote mbili kupambania nafasi ya kutinga hatua ya fainali.

Mshindi wa mchezo wa leo atakutana fainali na Express ambayo ilishinda nusu fainali ya kwanza Uwanja wa Azam Complex mbele ya KMKM kwa mabao 2-1.

Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Azam FC, Zakaria Thabit amesema kuwa wapo tayari kwa mchezo wa leo na wanahitaji ushindi ili kutinga hatua ya fainali.

SOMA NA HII  UWANJA WA AZAM COMPLEX KUFANYIWA MABORESHO MENGINE MAKUBWA