MSHAMBULIAJI wa Yanga, Heritier Makambo amesema kuwa anauhakika wa kufanya vizuri ndani ya Ligi Kuu Bara na atafunga kila anapopata nafasi.
Nyota huyo aliibuka Yanga baada ya kusitisha mkataba wake na Horoya AC ya Guinea. Alicheza Yanga msimu wa 2017/18 kabla ya kusepa na kuibukia nchini Guinea. Amerejea Yanga na kusaini dili la miaka miwili.