Home Habari za michezo KISA KUIFUNGA YANGA….RAIS SAMIA ASHINDWA KUJIZUIA…AONYESHA ‘MAHABA’ KWA SIMBA…

KISA KUIFUNGA YANGA….RAIS SAMIA ASHINDWA KUJIZUIA…AONYESHA ‘MAHABA’ KWA SIMBA…

Habari za Simba

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amewapongeza klabu ya Simba SC kwa kuibuka na ushindi katika mechi dhidi ya wapinzani wao wa jadi, Yanga SC.

Simba iliibuka na ushindi wa goli 2-0 jana katika mechi hiyo ya Ligi Kuu iliyopigwa katika Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar ambapo magoli hayo yaliwekwa kambani na beki Henock Inonga na Kibu Denis.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Rais Samia aliweka ujumbe huo.

“Hongereni Simba kwa ushindi wenu dhidi ya Yanga katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara. Upinzani wenu wa jadi uwanjani ni burudani inayowaleta pamoja mamilioni ya Watanzania katika kila kona ya nchi yetu, kwa namna ya kipekee. #KariakooDerby.”

SOMA NA HII  BAADA YA KUWAKOSA WAARABU...BOCCO ASHUSHA 'PRESHA' SIMBA..DAKTARI AFUNGUKA A-Z...