JAMES Ssetupa kipa namba moja wa Biashara United amesema kuwa anamshukuru Mungu kwa kumpa nguvu ya kufanya vizuri kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Simba uliochezwa Uwanja wa Karume, Mara ambapo aliweza kuikoa penalti ya nahodha wa Simba, John Bocco na kuwafanya wagawane pointi mojamoja.