Home kimataifa SAKATA LA MESSI KUSEPA BARCELONA LAIBUA MAPYA..RAIS WA LA LIGA ABWAGA ‘MBOGA’

SAKATA LA MESSI KUSEPA BARCELONA LAIBUA MAPYA..RAIS WA LA LIGA ABWAGA ‘MBOGA’


JAVIER Tebas, Rais wa La Liga ameweka wazi kuwa kusepa kwa nyota wao wa zamani Lionel Messi katika ligi hiyo ni maumivu makubwa lakini ilikuwa haiwezi kuepukika kwa kuwa hata Barcelona wenyewe walikataa mbinu waliyopewa ili abaki.

Messi alishindwa kusaini dili jipya ndani ya timu yake ya Barcelona huku sababu kubwa ikitajwa kuwa ni sheria za La Liga katika matumizi ya mkwanja.

Licha ya nyota huyo kuwa tayari kupunguza mshahara wake kwa asilimia 50 mambo yalikuwa magumu kwake na amesepa kwa sasa yupo zake ndani ya kikosi cha PSG.

Tebas amesema kuwa waliwapa chaguo Barcelona ambalo lingewafanya abaki kwao ila walikataa mwisho wa siku ameacha maumivu katika La Liga.

“Kama wangekubali, Messi alikuwa na uwezo wa kubaki kuwa Barcelona wala asingeondoka,”.

SOMA NA HII  MANCHESTER CITY YAICHAPA PSG NUSU FAINALI UEFA CHAMPIONS LEAGUE