Home news SALAMA JABIR AACHA KAZI EATV…ATAJWA KUWA NDIYE MSEMAJI MPYA SIMBA SC

SALAMA JABIR AACHA KAZI EATV…ATAJWA KUWA NDIYE MSEMAJI MPYA SIMBA SC


Mtangazaji nguli nchini na kipenzi cha wengi, Salama Jabir jana alitangaza kuachana na kituo cha EATV ambacho amefanya kazi hapo kwa muda wa takribani miaka 19 huku sababu kuu ikiwa ni kwenda nje ya media hiyo kuona pia hali ikoje.

Salama amekuwa EATV kwa muda mrefu akijizolea umaarufu zaidi na vipindi kama Mkasi βœ‚, Shabiki On Saturday (SOS) pamoja na kipindi cha SALAMA NA..

Lakini tetesi zimekuwa nyingi mitandaoni kuwa uwenda akawa msemaji wa klabu ya Simba SC japo mwenyewe amekataa kuwa si kweli na yeye anaziona habari hizi kwenye mitandao ya kijamii kama tunavyoona sisi.

Lakini tayari imeshaelezwa kuwa Salama kwa sasa anafanya kazi kwenye Kampuni MultiChoice kupitia king’amuzi chao cha DStv.

SOMA NA HII  UNAAMBIWA HUYO YAO HAPO JANGWANI NI ZAIDI YA JESHI