Home Azam FC BAADA YA KUANZA KUFUNGA FUNGA SANA….’FEI TOTO’ AJIPA MAZIMA UFALME WA YANGA

BAADA YA KUANZA KUFUNGA FUNGA SANA….’FEI TOTO’ AJIPA MAZIMA UFALME WA YANGA


KIUNGO wa Yanga, Feisal Salum ‘Fei Toto’ amefunguka kuwa bado anaiona nafasi yake katika kikosi cha timu hiyo kutokana na malengo aliyojiwekea kwamba anahitaji kufanya vizuri zaidi ya sasa.

Fei Toto ameanza msimu huu vizuri huku akiwa kinara wa mabao kwenye kikosi hicho ndani ya Ligi Kuu Bara akifunga mawili.

Akizungumza na Gazeti la Spoti Xtra, Fei Toto alisema: “Kila mchezaji anahitaji kuwa na nafasi kubwa ya kuanza katika timu, hivyo kwa upande wangu naiona nafasi yangu katika kikosi cha Kocha Nabi (Nasreddine) kwani nahitaji kufanya vizuri zaidi.

“Mipango yangu msimu huu ni kuhakikisha nafunga mabao mengi ili kuwa kinara wa mabao na kuipatia timu yangu ubingwa.”

SOMA NA HII  HUU HAPA MSIMAMO WA SIMBA KUHUSU 'KUCHEZA MECHI NNJE YA UWANJA'...MATOKEO YATAJWA...