Home news YANGA KUSHUKA UWANJANI LEO MBELE YA JKU SC

YANGA KUSHUKA UWANJANI LEO MBELE YA JKU SC


LEO Oktoba 10 kikosi cha Yanga kinachonolewa na Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi kinatarajiwa kujipima ubavu na timu ya JKU  SC katika mchezo wa kirafiki unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Azam Complex.

Wachezaji ambao wamebaki kambini Dar katika kijiji cha Avic Town ikiwa ni pamoja na Mayele, Abdul Shaibu, ‘Ninja’, Paul Godfrey, ‘Boxer’ watakuwa na kazi ya kujiweka sawa na kuonyesha uwezo wao.

Mchezo huo wa kirafiki unatarajiwa kuchezwa majira ya saa 1:00 usiku na utakuwa live Azam TV.

Kwa upande wa kiingilio kwenye mchezo huo mzunguko ni buku tatu pekee, (3,000) na VIP 5,000,(buku tano).

Mastaa ambao wapo kwenye majukumu yao ya taifa ikiwa ni pamoja na Dickson Job, Bakari Mwamnyeto, Feisal Salum hawa hawatakuwepo kwenye kikosi cha leo.


SOMA NA HII  RASMI...TARAHE YA MORRISON KUTAMBULISHWA YANGA HII HAPA...AWATUMIA KIJEMBE MASHABIKI WA SIMBA ...