Home news WAKATI YANGA WAKIMTAKA NGUSHI…MBEYA KWANZA WAIBUKA NA HILI…

WAKATI YANGA WAKIMTAKA NGUSHI…MBEYA KWANZA WAIBUKA NA HILI…


WAKATI kukiwepo na tetesi za Yanga kumuhitaji straika Chrispin Ngushi, mabosi wa straika huyo Mbeya Kwanza wameibuka na kubainisha kuwa wapo tayari kumuachia nyota huyo kutua Jangwani.

Ngushi amekuwa na msimu mzuri hadi sasa akiwa na Mbeya Kwanza ambapo ameweka kambani mabao matatu na asisti moja.

Akizungumza na gazeti la  Championi Jumamosi, Mwenyekiti wa Mbeya Kwanza, Mohammed Mashango alisema kuwa endapo Yanga watakuwa tayari kwa ajili ya mazungumzo basi wao kama timu watamuachia mchezaji huyo.

“Hadi sasa bado hatujapata ofa yoyote kutoka kwa Yanga lakini tumekua tukisikia kuwa wanamuhitaji lakini bado hawajafika kwetu kama wakija tukafanya mazungumzo na tukafikia makubaliano mazuri basi kila kitu kitakuwa wazi.

“Sisi kama timu tupo tayari kumuachia Chrispin kwenda Yanga kwani lengo letu ni kuona vijana wetu wanakuza vipaji, kwa hiyo hatutakuwa na pingamizi kwenye jambo hilo,” alisema Mashango.

SOMA NA HII  MAFAZA WAIBEBA SIMBA KWA MKAPA...GAMONDI ATAMBIA REKODI YA 5G...