Home news BEKI WA SIMBA ASHINDWA KUJIZUIA KUHUSU MAYELE…AFUNGUKA JINSI ALIVYOMTESA PAMOJA NA ‘KUMCHEZEA...

BEKI WA SIMBA ASHINDWA KUJIZUIA KUHUSU MAYELE…AFUNGUKA JINSI ALIVYOMTESA PAMOJA NA ‘KUMCHEZEA KAZI CHAFU’


BEKI wa kati wa Simba anayekipiga kwa mkopo Mtibwa Sugar, Ibrahim Ame, amesema mshambuliaji wa Yanga, Mkongomani, Fiston Mayele ameshindikana huku akisisitiza amemkosesha usingizi.

Kauli ya beki huyo imekuja baada ya mchezo wa Ligi Kuu Bara kumalizika kwa Yanga kuwafunga Mtibwa mabao 2-0 juzi Jumatano kwenye Uwanja wa Manungu, Turiani mkoani Morogoro.

Ame alisajiliwa na Simba msimu uliopita akitokea Coastal Union ya Tanga ambaye msimu huu alitolewa kwa mkopo Mtibwa pamoja na Said Ndemla na Jeremiah Kisubi.

 Ame alisema kuwa kabla ya mchezo huo, alipewa jukumu la kumkaba Mayele kwa lengo la kutofunga, lakini imeshindikana baada ya kumruhusu mshambuliaji huyo kufunga bao. Ame alisema kuwa bao hilo alilofunga Mayele, limemfanya akose furaha na amani huku akishindwa kupata usingizi.

Ame ambaye alishindwa kuendelea na mchezo baada ya bao hilo kutokana na maumivu, alionekana akiwa chini nje ya uwanja akisononeka. “Mayele ni mshambuliaji hatari na wa kuchungwa akiwa uwanjani kutokana na kiwango chake bora.

“Nakumbuka kabla ya mchezo wetu huo, nilipewa jukumu la kutembea na Mayele kila sehemu kwa lengo la kutofunga, lakini ikashindikana na kupata upenyo akafunga.

“Kiukweli nilifanya jitihada nyingi za kutosha za kuhakikisha Mayele hafungi lakini nimeshindwa, alitumia nafasi moja aliyoipata kufunga, kiukweli siku yangu imeharibika baada ya bao hilo, sitaweza kupata usingizi,” alisema Ame.

SOMA NA HII  CHAMA AZUA GUMZO CCM KIRUMBA .....AFUNGA MJADALA KUHUSU MGOGORO KATI YAKE NA PABLO...