Kikosi cha Simba SC kimeanza Safari ya kurejea nchini kutokea Afrika ya kusini walikokwenda kwa ajili ya mchezo wa pili, Robo Fainali Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Orlando Pirates.
Simba wameondolewa katika mashindano hayo kwa mikwaju ya penati 4-3 dhidi ya Orlando Pirates usiku wa Jana katika Uwanja wa Orlando.
Urejeo huu ni ishara ya kuwa wanajiandaa kwa mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Mtani wake wa Jadi Yanga utakaopigwa April 30.