Home Habari za michezo BAADA YA ‘KUMVUTISHA PUNZI YA JOTO’ MSAUZI JANA….UONGOZI SIMBA WATOA NENO HILI...

BAADA YA ‘KUMVUTISHA PUNZI YA JOTO’ MSAUZI JANA….UONGOZI SIMBA WATOA NENO HILI KWA MASHABIKI…


Uongozi wa Mabingwa wa Soka Tanzania Bara Simba SC umetoa shukurani kwa Mashabiki na Wanachama wake, kufuatia kuitikia wito wa kufika Uwanja wa Benjamin Mkapa kuishangilia timu yao ilipokua ikicheza dhidi ya Orlando Pirates ya Afrika Kusini.

Jana Jumapili (April 17) Simba SC ilikua mwenyeji wa Orlando Pirates katika Uwanja wa Benjamin Mkapa, ikianza kampeni za kusaka tiketi ya kucheza Nusu Fainali Kombe la Shirikisho kwenye mchezo wa Mkondo wa Kwanza wa Robo Fainali.

Shukran za Simba SC kwa Wanachama na Mashabiki zimetolewa na Meneja wa Habari na Mawasiliano wa klabu hiyo Ahmed Ally kwa kuandika ujumbe mzito katika ukurasa wake wa Instagram.

Ahmed aandika: TUMEWAITA MKAITIKAAA

Ninyi ni watu bora sana

SOMA NA HII  KAZI IMEANZA YANGA.....GAMONDI ATAKA STRAIKA LA BILIONI 2.5...MABOSI YANGA WAKUNA KICHWA..