Msemaji wa Klabu ya Yanga, Haji Manara amewapiga dongo tena mahasimu wao, Simba baada ya kutoa sare nyingine ya bao 1-1 dhidi ya Geita Gold, mchezo uliopigwa juzi Jumapili katika Dimba la CCM Kirumba jijini Mwanza.
Manara ameandika haya Kupitia Instagram:
“Sio mbaya mtajipanga Kwa Miaka ijayo mkipata akili na kupunguza uchawi.
Halaf Wananchi mbona mna siri sana, kumbe katika mechi sita zilizopita za Makolo, wameshinda mechi moja tu na sare tano? Halafu hamsemi????
Makolo 0 Polisi 0
Makolo 0 Yanga 0
Makolo 2 Namungo 2
Makolo 4 Ruvu 0
Makolo 1 Azam 1
Makolo 1 Geita 1
Halaf na nyie wa Michongo mmeuchuna kimyaaaaaa,Yanga tulitoa Sare Tatu tu, kelele kibao na mkatuandikia makala za kila aina.
Kwanza mlinielewa niliposema mwanzo wa msimu lile neno Return of the Champions?
Na ole wenu leo tukute Majivu CCM Kirumba.
Che Che Che
Wanayaona Macho yao
Pumzi ya Kitonsa.