Wafalme wa Ulaya, Real Madrid kwa mara nyingine wamefanikiwa kunyakua Kombe la Ligi ya Mabingwa barani Ulaya mbele ya majogoo wa Jiji Liverpool kwa ushindi wa goli 1-0.
Mchezo huo ambao ulikuwa unapigwa katika Jiji la Paris nchini Ufaransa, umewapa Real Madrid taji lao la 14 katika historia ya Michuano hiyo.
Goli la pekee na la ushindi la Madrid limewekwa wavuni na Winga wake Vinicious Junior dakika ya 59 ya mchezo.
Nyota wa mchezo wa leo anaki kuwa Mlinda mlango wa Real Madrid, Thibaut Curtois ambae alifanya kazi ya ziada tangiu kipindi cha kwanza kucheza na michomo ya Salah na Mane.