Home Habari za michezo COASTAL UNION WACHOMOZA MSAFARA WA KOMBE LA YANGA LEO…WAIMBWA KILA KONA YA...

COASTAL UNION WACHOMOZA MSAFARA WA KOMBE LA YANGA LEO…WAIMBWA KILA KONA YA JIJI…MASHABIKI HAWAELEWI KITU…


Bado Coastal …bado Coastal…bado Coastal’, hivi ndivyo mashabiki wa Yanga wakiimba wakati wakipokea taji lao la ligi.

Mashabiki hao wameipiga mkwara Coastal Union wakati wakiwa kwenye msafara wa kupokea kombe lao la ubingwa wa Ligi Kuu Bara.

Yanga imerejea asubuhi ya leo ikitokea jijini Mbeya ambapo wamekabidhiwa rasmi kombe hilo baada ya mchezo wao dhidi ya Mbeya City, ukimalizika kwa sare ya bao 1-1.

Mashabiki hao wakiwa wanakimbia barabarani kupokea kombe hilo wamekuwa wakiimba nyimbo wakidai bado Coastal Union.

Nyimbo hiyo ni sawa na kuipiga mkwara Coastal Union ambao watakutana nao Julai 2, kwenye Fainali ya Kombe la Azam Shirikisho.

Mchezo huo ambao utapigwa jijini Arusha kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, Yanga itakuwa inawania taji la tatu msimu huu.

Msimu huu tayari Yanga imeshachukua mataji mawili ya Tanzania bara wakitangulia kuchukua Ngao ya Jamii baada ya kuwachapa Simba,kisha jana kuchukua lile la ligi.

SOMA NA HII  KUHUSU SIMBA KUTUMIA BILIONI 3 KWA KIPA MPYA....?, UKWELI WOTE HUU HAPA...