Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani FIFA, Gianni Infantino, ameipongeza Klabu ya Yanga kwa kunyakua Ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2021/2022.
Katika Taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Mpira nchini TFF, imesema kuwa Infantino amesifu juhudi na umoja uliooneshwa na Klabu ya Yanga.
Yanga wamebeba Ubingwa baada ya kupita miaka minne, na siku ya Juni 26 walifanya mapokezi yaliyowashangaza wapenda Soka katika maeneo mbali mbali duniani.
Soma kwa kirefu taarifa ya TFF;