Home Habari za michezo A-Z JINSI MASTAA WATANO SIMBA WALIVYOPOKELEWA KWA ‘VIBE’ LA AINA YAKE NA...

A-Z JINSI MASTAA WATANO SIMBA WALIVYOPOKELEWA KWA ‘VIBE’ LA AINA YAKE NA WENZAO MISRI…


Nyota watano wa Simba SC waliokuwa wamesalia jijini Dar, tayari wamewasili kambini Ismailia Misri kuungana na wenzao ambao walishatangulia nchini humo kwa ajili ya pre season.

Nyota hao ni Tadeo Lwanga, Peter Banda, Henock Inonga, Moses Phiri na Nassoro Kapama ambapo video iliyoachiwa na Simba SC, imewaonesha wakipokeleza na wenzao wakiwa wanapata chakula.

Kikosi cha Simba kilichoweka kambi chini ya kocha Zaron Maki, jana kilicheza mchezo wa kirafiki na na timu ya Ismaily ambapo walitoka sare ya 1-1.

Simba wanatarajia kurejea nchini Agosti 5, 2022 kwa ajili ya kuanza msimu mpya wa ligi ambapo Agosti 13 itakuwa ndio mechi ya ufunguzi wa ligi na Simba atapepetana na Yanga.

SOMA NA HII  KARIAKOO DABI: HAKUNA MBABAE.....YANGA YABAKI NA ZAKE..SIMBA WAENDELEA NA ZAO...