Baada ya sintofahamu ya taarifa ya mshambuliaji wa @Geitagoldfc George Mpole kusambaa mitandaoni ikisema amegoma kuungana na timu hiyo na mkataba wake umekwisha, mchezaji huyo ameonekana mazoezini na matajiri hao wa dhahabu katika maandalizi ya mchezo wa ligi kuu ya NBC dhidi ya @simbasctanzania utakaopigwa siku ya kesho Agosti 17, 2022 katika Dimba la Mkapa.