Timu ya Simba Queens imepangwa Kundi A katika Ligi ya Mabingwa Afrika pamoja na ASFAR ya Morocco,Green Buffaloes ya Zambia na Determines Girls ya Liberia.
Katika michuano hiyo itakayoanza Oktoba 30 hadi Novemba 13 nchini Morocco, Kundi B linaundwa na mabingwa watetezi, Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini, Bayelsa Queens ya Nigeria, Wadi Degla ya Misri na mwakilishi wa ukanda wa UNIFFAC.