Home Habari za michezo YANGA WAITAKA REKODI YA ARSENAL…WAKISHINDA KESHO KUTWA….WANAINGOJA DODOMA TU…

YANGA WAITAKA REKODI YA ARSENAL…WAKISHINDA KESHO KUTWA….WANAINGOJA DODOMA TU…

Kikosi cha Yanga SC

Yanga SC imesafiri Hadi Mkoani Singida kucheza na Dodoma Jiji kesho kutwa Novemba 23, endapo Yanga atashida Mchezo huo atakuwa anaikaribbia rekodi kama ya Arsenal Mwaka 2003 May 7, The Gunners walicheza Mechi 49 Bila kupoteza mpaka Oktoba 16, 2004

Yanga wako Mkoani Singida kuzitafuta alama tatu kwenye uwanja wa Liti, watakapokuwa na kibarua kingine dhidi ya walima Zabibu, Dodoma Jiji FC. Mchezo huo utachezwa Jumanne Novemba 22/2022.

Young Africans ipo nafasi ya pili kwenye msimamo wa Ligi, baada ya kushushwa na watani zao Simba SC kwa utofauti wa alama moja, ambayo Simba wana alama 27 na Yanga anazo 26 na michezo michache zaidi ya Simba.

Kabla ya Wananchi kusafiri walicheza kwanza mchezo wa kirafiki na timu ya Vijana ya Klabu hiyo, na kuibuka na ushindi wa bao 3-2. Hiyo ilikuwa ni maandalizi ya kujiweka sawa kwa mchezo huo ambao Yanga atahitaji kushinda ili arudi kileleni mwa Ligi na kuendeleza rekodi yake ya kutopoteza kwenye michezo 47 na hivyo kuikaribia ile rekodi iliyowekwa na Arsenal ya mechi 49 bila kupoteza mwaka 2003-2004.

SOMA NA HII  MANARA TENAAH...ASHINDWA KUJIZUIA KUHUSU 'KAMATI KAMATI' ZA MSHINDO MSOLA..AMTAJA SENZO...