Home Habari za michezo SIMBA WAISHIKA PABAYA HOROYA…WANASA MIPANGO YAO YOTE….

SIMBA WAISHIKA PABAYA HOROYA…WANASA MIPANGO YAO YOTE….

Habari za Simba

Horoya akishinda Mechi yake na Raja Casablanca itakuwa ngumu kwa Simba kufuzu hatua ya Robo Fainal ya Kombe la Mabingwa Afrika hata Kama Simba atashinda Mechi zake zote.

Moja kati ya mikakati ya Kuhakikisha Wanashinda Rais wa klabu ya Horoya Soufiane Souare atangaza kitita.

Horoya na Raja Casablanca zinashuka dimbani wiki ijayo kwenye mwendelezo wa michuano ya CAFCL raundi ya nne kundi C huku Raisi wa klabu hiyo Bilionaire Soufian Souare akitangaza dau kila goli kulinunua shilingi mil 100 kuanzia mchezo huo na itakayofuata ambapo itakuja Tanzania kucheza na Simba huku mechi ya mwisho ikiikaribisha Vipers.

Rais huyo anataka Horoya itinge robo fainali ya michuano hiyo kwa kushinda mechi zote zilizosalia kujihakikishia tiketi moja wapo kwenda robo fainali.

Kwa mantiki hiyo timu zote kundi C zina nafasi ya kutinga robo fainali itategemea zimejipanga vipi kumaliza mechi 3 zilizobakia kila timu inatakiwa kuzichanga karata zake vizuri kutimiza malengo yao.

Hivyo Horoya akishinda Mechi ya Raja Na Vipers atafuzu Robo Fainal Caf Champions league Hapa Sasa Hivi Wanasimba tuwaombee Raja washinde hii Mechi au watoe Sare pengine Simba akishinda Mechi zake atafuzu.

SOMA NA HII  KOCHA TAIFA STARS:- NATEGEMEA UGANDA WATABADILIKA KATIKA MECHI HII...LAZIMA WAFE KIFO CHA MENDE